WIRE โ€” Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko ameanzisha tena mashambulizi dhidi ya Mahakama ya Juu, akihoji jinsi ilivyoshughulikia rufaa yake kuhusu kung'olewa madarakani na kudokeza kuwa anajiandaa kuwasilisha ombi jipya la mapitio ya uamuzi huo akitegemea kile alichokitaja kuwa ushahidi mpya na wa kushawishi. Katika taarifa ya kina aliyoitoa Alhamisi, Sonko alihoji kwa nini Mahakama ya Juu sasa inataka ushauri kutoka kwa Mwanasheria Mkuu Dorcas Oduor kuhusu iwapo afisa wa umma aliyeng'olewa madarakani anaweza kugombea uchaguzi wakati rufaa yake bado inaendelea, ilhali mahakama hiyo tayari ilitoa msimamo kuhusu suala hilo katika kesi yake. "Swali langu kwa Mahakama ya Juu, hasa kwa Jaji Mkuu, ni hili: Kwa nini iombe ushauri kutoka kwa Mwanasheria Mkuu Dorcas Oduor kuhusu iwapo maafisa wa umma waliotimuliwa wanaweza kugombea uchaguzi wakati kesi zao bado zinaendelea, ilhali Mahakama ya Juu tayari ilitoa uamuzi kuhusu kung'olewa kwangu? Zaidi ya hayo, kwa nini itafute ushauri huo ilhali Jaji Mkuu alikuwa tayari amesema hadharani, siku chache kabla ya hukumu ya rufaa yangu, kwamba gavana aking'olewa hubaki ameng'olewa?" alihoji Sonko. Sonko pia alirejelea matukio yaliyotangulia uamuzi wa Mahakama ya Juu wa Julai 2022 uliothibitisha kuondolewa kwake madarakani. Alidai kuwa ย Jaji Mkuu Martha Koome alisema hadharani, wakati rufaa yake bado ilikuwa ikiendelea, kwamba gavana aking'olewa hubaki ameng'olewa. Kwa mujibu wa Sonko, aliwasilisha ombi rasmi akimtaka Jaji Mkuu ajiondoe katika kesi hiyo kwa madai kuwa kauli hizo zilionyesha upendeleo, lakini ombi lake lilikataliwa. "Wakati rufaa yangu ilikuwa bado inasikilizwa Mahakama ya Juu, Jaji Mkuu alisema katika mahojiano na Spice FM kwamba gavana aking'olewa hubaki ameng'olewa. Kwa kuwa kesi ilikuwa bado haijaamuliwa, niliona kauli hizo zilitoa taswira kwamba uamuzi ulikuwa tayari umefikiwa. Niliandika nikitaka ajiondoe katika kesi hiyo lakini alikataa na akaendelea kushiriki katika kutoa hukumu. Hilo linanifanya niulize: Je, uamuzi kuhusu rufaa yangu ulikuwa tayari umeamuliwa?" alisema. Pia alihoji msururu wa matukio yaliyoishia na hukumu ya Mahakama ya Juu. Alisema kuwa mnamo Julai 13, 2022, Mahakama Kuu ya Mombasa iliamua kwamba kwa kuwa rufaa yake Mahakama ya Juu ilikuwa bado haijakamilika, alikuwa hajamaliza njia zote za kisheria na hivyo alikuwa na haki ya kuidhinishwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kugombea ugavana wa Mombasa. Hata hivyo, Sonko alisema Mahakama ya Juu ilimwagiza kuwasilisha hoja zake ndani ya saa chache akiwa bado katika Mahakama Kuu ya Mombasa, ikasikiliza kesi hiyo ย Julai 14 na kutupilia mbali rufaa yake Julai 15. "Kinachonisumbua zaidi ni kilichotokea Julai 13. Nilipokuwa Mahakama Kuu ya Mombasa siku nzima, Mahakama ya Juu ilitoa maagizo kwamba niwasilishe hoja katika rufaa yangu ifikapo Julai 14. Mawakili wangu walieleza mahakama kwamba tulikuwa katika kesi nyingine na tukaomba muda unaotolewa kwa kawaida chini ya taratibu za mahakama. Ingawa mahakama ilikiri kulikuwa na hitilafu katika muda uliowekwa, bado iliendelea na kesi hiyo," alisema. Sonko alisisitiza kuwa kung'olewa kwake kulichochewa kisiasa. Alidai kuwa baadhi ya waliowasilisha na kuunga mkono hoja ya kumwondoa madarakani baadaye walijitenga nayo hadharani na kudai walifanya hivyo chini ya shinikizo. Kwa maoni yake, matukio hayo yanazua maswali mapya kuhusu uadilifu wa mchakato mzima wa kumng'oa madarakani. Pia alinukuu uamuzi wa Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ), akisema mahakama hiyo ilibaini mapungufu ya kiutaratibu katika jinsi kesi yake ilivyoshughulikiwa. Kwa mujibu wa Sonko, mahakama hiyo ya kikanda iliamua kuwa baadhi ya hatua zilizochukuliwa zilikiuka haki yake ya kupata kesi ya haki chini ya Katiba ya Kenya na hazikuendana na misingi ya utawala bora, utawala wa sheria na uwajibikaji iliyoainishwa katika Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sonko alisema masuala anayoyaibua hayahusu kesi yake pekee, bali yanagusa uhuru wa mahakama, uwazi na imani ya wananchi kwa mfumo wa haki. "Maswali yangu kwa Mahakama ya Juu ni rahisi. Kwa nini kauli ย zilitolew hadharani kuhusu kesi iliyokuwa bado mahakamani? Kwa nini ombi langu la Jaji Mkuu kujiondoa lilikataliwa? Kwa nini nilipewa saa chache tu kuwasilisha hoja badala ya muda wa kawaida? Kwa nini kulikuwa na haraka ya kumaliza rufaa yangu wakati suala la kustahili kwangu kugombea ugavana wa Mombasa lilikuwa bado linashughulikiwa na mahakama nyingine? Na sasa kwa nini Mwanasheria Mkuu anaombwa kutoa ushauri kuhusu jambo ambalo Mahakama ya Juu tayari iliamua katika kesi yangu?" alihoji. .

"We aggregate wires to encourage regional discovery, sending readers directly back to the original source to explore full coverage."

This is a normalized overview of the breaking feed event. The complete, official release detailing all points, background context, and statements remains hosted by the original publisher.