WIRE โ KIONGOZI wa DCP Rigathi Gachagua amewataka wafuasi wake wakome kumshambulia Naibu Rais Profesa Kithure Kindiki, kauli ambayo imefasiriwa kuwa wanasiasa hao wamechukua mkondo wa maridhiano. Bw Gachagua ambaye amekuwa mkosoaji wa naibu rais alisema hakuna haja ya kumshambulia Profesa Kindiki ilhali pia anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa wanasiasa wanaomezea mate kiti chake. Aidha Bw Gachagua alisema yupo karibu kumkaribisha Profesa Kindiki nyumbani iwapo ataishia kukosa kuwa mgombeaji mwenza wa Rais Ruto mnamo 2027 huku akisisitiza kuwa eneo la Mlima Kenya lazima lisalie limeungana licha ya tofauti za kisiasa. Kauli yake ilikuja wiki moja baada ya Profesa Kindiki kumkemea Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku kuhusu matamshi yake kuwa Mlima Kenya Mashariki utajitenga na wenzao wa Magharibi na kupiga kura kivyake mnamo 2027.
"We aggregate wires to encourage regional discovery, sending readers directly back to the original source to explore full coverage."
This is a normalized overview of the breaking feed event. The complete, official release detailing all points, background context, and statements remains hosted by the original publisher.